..
|
Nani
Afaidikaye Tokana Vitendo Vyako?
|
........
|
Vitoleo
vya mafunzo.
Kuwa
mtafiti wa jamii na mchanganuzi;
Mfinyanzi
shupavu lazima ajue sifa bainifu ya udondo
|
..
| Methali
nyingine itumikayo katika uwezeshaji wa jamii ni “Mfinyanzi lazima aujue
udongo wake.” Udongo wako ni jamii. Unataka kuifinyanza, uiendeleze
ipate nguvu. |
. |
Ili
ufaulu kufanya hivyo lazima ujue na kuifahamu vyema hiyo jamii (na
pia ujue na kufahamu hali ya jamii kijumla). Lazima ujue mengi iwezekanavyo
kuhusu mpangilio wa hiyo jamii, uchumi wake, lugha zake, matatizo yake,
siasa zake, ramani zale na ikolojia yake. |
..
| Utafiti
wako usiwe tu hutafuta orotha ya mambo ambayo hayahusiani; utahitaji kuyachanganuza
hadi uelewe kina cha jamii hama mfumo wa ujamaa. |
. |
Waza
kuhusu jinsi elementi tofauti zinahusiana. (Tazama “Jamii
ni nini?” Na “Utafiti wa Jamii”). (See What
is Community? and Social Research). |
..
| Mwanzo
mzuri ni kuchora ramani (map). Watu wanaishi
wapi? Kuna huduma gain kati ya hiyo jamii? (kama barabara, vichochoro,
mitambo ya maji, kliniki, shule, usafi afya, soko na huduma zinginezo). |
. |
Baadaye,
utakopo waongoza (assessment) wana jamii kwa
ukadiriaji wa wa hali yao (rasilimali, mahitaji, mafaa na shida),
utawaongoza kuchora ramani ya kijamii. Ukichora yako binafsi sasa, utasaidika
kwa matayarisho ya hiyo ramani ya pamoja baadaye. |
..
| Andika
muhtasari wako kwenye shajara. Eleza maoni yako kuhusu: mpangilio wa jamii,
uchumi, lugha, siasa, thamana za mgao, tamaduni, na uhusiano wao wa kimaumbile
na mazingira (ikolojia). |
. |
Endelea
kuchanganuza jinsi elementi tofauti zinahusiana. |
..
| Utajifunza
ya kwamba jamii (community) sio
tu mkusanyiko wa watu binafsi lakini ni mfumo unaopita mipaka ya hao watu
binafsi. Kama mfumo jamii ina vipimo kadhaa, vya kiteknolojia (technological),
via kiuchumi, vya kisiasa, via jingo la ustawi wa jamii (institutional),
via itikadi (ideological) na kimawazo,
Watu huja na kuondoka katika jamii, kwa kuzaliwa (economic),
kifo na uhamiaji (political),
na hata hivyo mfumo unashikilia. Huu mfumo hubadilika kila wakati. |
. |
Kazi
yako ni kuelewa huu mfumo ili uweze kuashiria kwa kudukua (nudge) hayo
mabadiliko na kuyaelekeza upande fulani (kama ilivyoelezwa kwenye vikomo
vyako ambavyo tulivijadili awali). |
..
|
Kuna
chungu nzima ya kujifunza kuhusu jamii unayolenga na haifai kukomesha
hayo mafunzo.
|
––»
«––
|